Jiunge

Jiunge MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection

Unayo account ? Log In


Unayo account ? Log in

Log In

Login MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection

Jiunge Hapa


Umesahau Password?

Hauna Account, Jiunge Hapa

Umesahau Password

Umesahau password yako?. Andika email yako hapo chini alafu bonyeza 'Reset'. Utapokea link katika email yako kwa ajili ya kutengeneza password mpya.

Unayo account ? Log in

Tafadhali andika jina lako kamili.

Tafadhali andika E-Mail yako.

Please choose an appropriate title for the question so it can be answered easily.


Tafadhali elezea kwa nini unahisi chapisho hili linapaswa kuripotiwa

Sign InSign Up

1Sky

1Sky

1Sky Navigation

  • Blog
  • Wasiliana Nasi
  • Advanced Search
  • App

Mobile menu

Close
Uliza Swali
  • Home
  • Maswali
  • Points
  • Miongozo
  • Wasiliana Nasi
  • Advanced Search
  • App
Home» Maswali»Q 32325
In Process
Poll
Anonymous
Asked: June 12, 20192019-06-12T09:33:35+03:00 2019-06-12T09:33:35+03:00Ukristo

Yesu ni Mungu?

Poll Results

100%Ndio ( 2 )
0%Hapana ( 0 )
Based On 2 Votes

Yesu ni Mungu?

Yesu ni Mungu?
  • 1
  • 552
  • 0
  • Share
    • Share on WhatsApp
    • Share on Facebook
    • Share on Twitter
Jibu
  • Report

Jibu 1

  • Kura
  • Zamani
  • Mpya
  1. Emmanuel Magessa

    Emmanuel Magessa

    • Mbeya, Tanzania
    • 1 Question
    • 32 Answers
    • 0 Best Answers
    • 69 Points
    View Profile
    Emmanuel Magessa Intermediate
    2021-03-31T21:15:51+03:00Jibu - March 31, 2021 saa 9:15 pm

    Haya ni maoni ya mdau asiyependa jina lake lijulikane. Nimeyatundika hapa kwa sababu ya uzito wa anachokisema. Tafadhali soma na kama unaweza changia maoni yako tuelimike.

    Nimshukuru sana kwa kutumia muda wake kuandika maoni yake na hapa namnukuu:

    MAKANISA ya Kikristo yanafunza ya kuwa Yesu Kristo si kama kuwa ni Mwana wa Mungu tu, bali hakika ni Mungu khasa. Baba, Mwana na Roho Mtakatifu ni mmoja. Watatu katika mmoja, na mmoja katika watatu. Wote ni wa milele, wote ni sawa. Yesu ni Mungu, na Mungu ni Yesu. Hiyo ni imani ya Kikristo, ambayo inaaminiwa na karibu Wakristo wote. Hebu tuifunue Biblia tutazame inasema nini katika jambo hili?
    Mt Paulo katika barua yake ya kwanza kuwapelekea Wakorintho aliandika:

    Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi.
    1 Wakorintho 15.15

    Juu ya kuwa Paulo anaambiwa ya kuwa akiamini kuwa Masihi (yaani Kristo) na Mwenyezi Mungu ni kitu kimoja hapa anasema: “Tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo.” Ikiwa Mungu kamfufua Kristo, hawawezi kuwa wote wawili hao ni mtu mmoja. Mmoja alikuwa ni mtenda, mfufuaji, na wa pili alikuwa ni mtendwa, mfufuliwa. Kama Kristo ni Mungu mwenye uwezo wa kufufua basi maelekeo ni kusema: “Kristo kajifufua”, sio kafufuliwa. Mwenye kufufuliwa ni mfu asiyejiweza kitu.
    Katika kitabu cha Matendo ya Mitume inasimuliwa kuwa Mt Stefano alisema aliyoyaona yaliyo mbinguni. Alisema:

    Tazama! naona mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adamu amesimama mkono wa kuume wa Mungu.
    Matendo 7.56

    Mwana wa Adamu ndiye Yesu, na kwa jina hilo ndio mwenyewe akipenda kujiita, sio Mwana wa Mungu. Hapo basi huko mbinguni Stefano anasema anamwona Yesu kakaa mkono wa kulia wa Mungu. Mwenye kukaa mkono wa kulia wa fulani hawezi kuwa ndiye yule yule fulani. Hayo ni maelezo ya mbinguni. Ni wazi basi kwa ushahidi wa Biblia kuwa Yesu hakuwa Mungu mbinguni kama alivyokuwa si Mungu duniani.
    Yesu alipokimbilia kwenye Mlima wa Zaituni na huku akisakwa na Mayahudi alijitenga na wanafunzi wake. Huko faraghani aliomba hivi:

    Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke. Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.
    Luka 22.42-43

    Hapa tunaona mambo matatu muhimu:

    Yesu anamwomba Mungu. Yesu anamwabudu Mungu. Wawili hao ni mbali mbali, na vyeo vyao ni mbali mbali. Yesu ni mtumwa mnyonge mwenye kuomba na kuabudu. Na Mungu ni Mwenyezi Mungu mwenye uwezo wote na mwenye kustahiki kuabudiwa pekee, hata na Yesu, mwenye kutakiwa msaada pekee, hata na Yesu.
    Mapenzi ya Mungu ni mbali na yale ya Yesu. Yesu hataki kuuliwa, ananyenyekea na kuomba kwa Bwana wake: “uniondolee kikombe hiki” cha mauti. Yesu hana azma hata chembe ya kufa msalabani, kifo cha mhalifu, kifo cha laana kama maadui zake Mayahudi walivyoazimia kumpatilisha nacho. Lakini anakiri kuwa ni mapenzi ya Mungu sio yake yeye yatendeke. Yeye hana hila wala nguvu za kuzuia kudra ya Mwenyezi Mungu.
    Yesu, Mwana wa Adamu, anakata tamaa. Imani inampunguka. Kavunjika moyo. Ikabidi “Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.”
    Jee, yaelekea kuwa Yesu ndiye Mungu? Yaelekea kuwa yeye na Mungu kuwa ni sawa? Kama upo wasiwasi wo wote wa kujibu hayo, mwenyewe Yesu anajibu kama anavyo hadithiwa na Yohana kuwa kasema:

    Baba ni mkuu kuliko mimi.
    Yohana 14.28

    Na mwishoni naye yupo msalabani:

    Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha?
    Mathayo 27.46

    Yafaa hapa tujiulize: Yesu akimlilia Mungu gani hapo msalabani ikiwa naye mwenyewe ni Mungu? Au nini alikusudia aliposema: “Mungu wangu naye ni Mungu wenu”? Maneno hayo kama yanaonyesha cho chote basi yanaonyesha unyenyekevu wa Yesu mbele ya Mungu wake. La kustaajabisha ni kule kukata tamaa kwake na kuvunjika moyo. Huwaje mtu wa imani, licha ya nabii na mwana pekee wa Mungu, akate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Ama kuwa Mungu akate tamaa na Mungu, na kumyayatikia: “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha”, ni jambo ambalo halimkiniki kuwa.
    Kwa uthibitisho ulio wazi Biblia inatwambia kuwa Yesu si Mungu, wala Mungu si Yesu.”

    Mwisho kunukuu.

    Kusoma original na kuendelea na hii discussion nenda 👉Bwaya blog

    • 0
    • Reply
    • Share
      Share
      • Share on WhatsApp
      • Share on Facebook
      • Share on Twitter
      • Report
Jibu swali hili

Jibu swali hili
Cancel reply

Chagua

Sidebar

Promo

  • Gugo kwa Kiswahili, Jaribu Sasa

  • Nafasi zote mpya za kazi zipo hapa

  • Tafuta vitu mtandaoni kwa lugha ya Kiswahili

  • Tafuta Ajira kiurahisi. Jaribu Sasa

  • Maswali Mengine

    • Katika 1 Timotheo 5:23, kwa nini mvinyo umeruhusiwa?

      • Majibu 0
    • Mistari ipi ya Biblia inaelezea maswala ya kodi?

      • Majibu 0
    • Ivi kusingekua na dini kungekuwa na dhambi?

      • Jibu 1
    • Kitabu gani cha Biblia kinamzungumzia Yesu?

      • Jibu 1
    • Nani alimsaliti Yesu?

      • Majibu 0
    • Nani alimkana Yesu?

      • Majibu 0
    • Nani aliandika kitabu cha Zaburi?

      • Majibu 2
    • Nani aliandika Biblia?

      • Majibu 0
    • Nini maana ya neema katika agano jipya?

      • Majibu 0
    • Tofauti kati ya mvinyo na divai ni nini?

      • Majibu 0

    Explore

    • Home
    • Maswali
    • Polls
    • Points
    • Watumiaji
    • Miongozo
    • App

    MojaSky

    Insert/edit link

    Enter the destination URL

    Or link to existing content

      No search term specified. Showing recent items. Search or use up and down arrow keys to select an item.