Jiunge

Jiunge MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection

Unayo account ? Log In

Unayo account ? Log in

Log In

Login MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection

Jiunge Hapa

Umesahau Password?

Hauna Account, Jiunge Hapa

Umesahau Password

Umesahau password yako?. Andika email yako hapo chini alafu bonyeza 'Reset'. Utapokea link katika email yako kwa ajili ya kutengeneza password mpya.

Unayo account ? Log in

Tafadhali andika jina lako kamili.

Tafadhali andika E-Mail yako.

Please choose an appropriate title for the question so it can be answered easily.

Tafadhali elezea kwa nini unahisi chapisho hili linapaswa kuripotiwa

Sign InSign Up

1Sky

1Sky

1Sky Navigation

  • Blog
  • Wasiliana Nasi
  • Advanced Search
  • App

Mobile menu

Close
Uliza Swali
  • Home
  • Maswali
  • Points
  • Miongozo
  • Wasiliana Nasi
  • Advanced Search
  • App

TRA

Share
  • Facebook
0
9Answers
9Questions
Home»Kodi»TRA
Adv
  • Maswali
  • Majibu
  • Majibu mengi
  • Bila jibu
  • Views nyingi
  1. Asked: November 19, 2019TRA

    Nawezaje kuwasiliana na TRA?

    Salim Jumbe

    Salim Jumbe

    • Dar es Salaam, Tanzania
    • 0 Questions
    • 127 Answers
    • 0 Best Answers
    • 436 Points
    View Profile
    Salim Jumbe Proffesional
    Jibu - April 11, 2021 saa 4:29 pm

    Wasiliana na TRA kwa njia hizi Msimbo wa Posta : 28 Edward Sokoine Drive, 11105 Mchafukoge, Ilala CBD, S.L.P 11491, Dar es salaam, Tanzania Simu:+255 22 2119591-4 Kituo cha huduma kwa Wateja  Tafadhali piga simu  kwa maswali, malalamiko na maoni. Wateja wote wa TRA wanahamasishwa kutumia huduma hiziSoma Zaidi

    Wasiliana na TRA kwa njia hizi

    Msimbo wa Posta : 28 Edward Sokoine Drive, 11105 Mchafukoge, Ilala CBD, S.L.P 11491, Dar es salaam, Tanzania

    Simu:+255 22 2119591-4

    Kituo cha huduma kwa Wateja 

    Tafadhali piga simu  kwa maswali, malalamiko na maoni. Wateja wote wa TRA wanahamasishwa kutumia huduma hizi popote pale walipo.

    Simu za Tanzania zitakuwa bure:

    0800 750 075

    0800 780 078

    Muda wa kazi Kituoni utakuwa kuanzia Saa 02:00 Asubuhi mpaka 01:00 Usiku kwa saa za Afrika Mashariki Jumatatu hadi Ijumaa isipokuwa siku za sikukuu.

    Ofisi za TRA za Mkoa

    Tafuta taarifa zote za mawasiliano kwa ofisi za mikoani hapa.

    • Kituo cha mawasiliano ya simu Mawasiliano ya TRA
      Dar es salaam, Tanzania
      Phone: 0800 750075 (Vodacom )
    • Arusha Meneja wa Mkoa
      Arusha, Tanzania
      Phone: +255 27 2502946
    • Mkoa wa Pwani Meneja wa Mkoa
      Kibaha
      Phone: +255 23 240 2905
    • Kinondoni Meneja wa Mkoa
      Dar es salaam
      Phone: +255 22 2771846
    • Ilala Meneja wa Mkoa
      Dar es salaam
      Phone: +255 22 2185545
    • Temeke Meneja wa Mkoa
      Dar es salaam
      Phone: +255 22 2861122
    • Mwanza Meneja wa Mkoa
      Mwanza
      Phone: +255 28 2500906
    • Tanga Meneja wa Mkoa
      Phone: +255 27 2642200
    • Kilimanjaro Meneja wa Mkoa
      Moshi
      Phone: +255 27 2753268
    • Tabora Meneja wa Mkoa
      Tabora
      Phone: +255 26 2604609
    • Rukwa Meneja wa Mkoa
      Sumbawanga
      Phone: +255 25 2801089
    • Ruvuma Meneja wa Mkoa
      Songea
      Phone: +255 25 2602140
    • Shinyanga Meneja wa Mkoa
      Shinyanga
      Phone: +255 28 2762385
    • Singida Meneja wa Mkoa
      Singida
      Phone: +255 26 2502320
    • Mtwara Meneja wa Mkoa
      Mtwara
      Phone: +255 23 2333662
    • Mbeya Meneja wa Mkoa
      Mbeya
      Phone: +255 25 2502165
    • Mara Meneja wa Mkoa
      Musoma
      Phone: +255 28 2622551
    • Manyara Meneja wa Mkoa
      Babati
      Phone: +255 27 2531006
    • Lindi Meneja wa Mkoa
      Lindi
      Phone: +255 23 2202662
    • Kigoma Meneja wa Mkoa
      Kigoma
      Phone: +255 28 2802054
    • Kagera Meneja wa Mkoa
      Bukoba
      Phone: +255 28 2220390
    • Iringa Meneja wa Mkoa
      Iringa
      Phone: +255 26 270144
    • Morogoro Meneja wa Mkoa
      Morogoro
      Phone: +255 23 261 4192
    • Dodoma Meneja wa Mkoa
      Dodoma
      Phone: +255 26 232 2912
    See less
    • 0
    • Share
      Share
      • Share on WhatsApp
      • Share on Facebook
      • Share on Twitter
      • Report
  2. Promo – MeridianBet

    Kubet kumerahisishwa

    Jipatie Tsh 3,500 ya kuanzia kama zawadi ya kujiunga.

    Jiunge Sasa
  3. Asked: February 4, 2020Biashara/Ujasiriamali, Kodi, TRA

    VAT Tanzania ni asilimia ngapi?

    Salim Jumbe

    Salim Jumbe

    • Dar es Salaam, Tanzania
    • 0 Questions
    • 127 Answers
    • 0 Best Answers
    • 436 Points
    View Profile
    Salim Jumbe Proffesional
    Jibu - February 4, 2020 saa 8:14 am

    Kiwango cha VAT kinachotumika Tanzania ni 18%

    Kiwango cha VAT kinachotumika Tanzania ni 18%

    See less
    • 0
    • Share
      Share
      • Share on WhatsApp
      • Share on Facebook
      • Share on Twitter
      • Report
  4. Promo – MeridianBet

    Kubet kumerahisishwa

    Jipatie Tsh 3,500 ya kuanzia kama zawadi ya kujiunga.

    Jiunge Sasa
  5. Asked: January 10, 2020Biashara/Ujasiriamali, TRA

    Masharti ya TRA yakoje katika kuanzisha biashara?

    Salim Jumbe

    Salim Jumbe

    • Dar es Salaam, Tanzania
    • 0 Questions
    • 127 Answers
    • 0 Best Answers
    • 436 Points
    View Profile
    Salim Jumbe Proffesional
    Jibu - January 10, 2020 saa 8:15 am

    Kupitia tovuti yao wameandika hivi Mtu Binafsi Mtu binafsi awe mkazi au si mkazi anatakiwa kutembelea ofisi ya TRA ya mkoa au wilaya na kujaza fomu ya maombi ya Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN). Maombi yanaweza kufanywa pia kwa njia ya mtandao, hata hivyo mwombaji lazima afike ofisi za TRA kwSoma Zaidi

    Kupitia tovuti yao wameandika hivi

    Mtu Binafsi

    Mtu binafsi awe mkazi au si mkazi anatakiwa kutembelea ofisi ya TRA ya mkoa au wilaya na kujaza fomu ya maombi ya Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN). Maombi yanaweza kufanywa pia kwa njia ya mtandao, hata hivyo mwombaji lazima afike ofisi za TRA kwa ajili ya kuchukuliwa alama za vidole pamoja na kupiga picha na kuweka saini.

    Baada ya kupata cheti cha namba ya utambulisho wa mlipakodi mwombaji atatakiwa kuomba leseni ya biashara kutoka ofisi za Biashara katika Wilaya, Manispaa, Jiji na Wizara ya Biashara na Viwanda kwa kutegemea aina ya biashara anayotaka kuanzisha.

     

    Hati ya Usajili:

    Mtu binafsi anaweza kuamua kusajili jina la biashara kwa wakala aliyepewa kazi hiyo na Wizara ya Biashara na Viwanda anayejulikana kama Mamlaka ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Jina lililosajiliwa linaweza kupatikana kabla au baada ya kutoa maombi ya TIN. Jina la biashara lililosajiliwa litaonyeshwa kwenye hati ya TIN pamoja na jina la mtu huyo ikionyesha jina la mmiliki wa biashara kama (T/A).

     

    Shirika (kampuni yenye dhima ya ukomo)

    Kuanzisha shirika kunahitaji mtu aombe kupatiwa Hati ya shirika kutoka Mamlaka ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Wahamasishaji wa kampuni wanatakiwa kuandaa na kuwasilisha hati  na Mkataba na kanuni za kampuni.

    Hati ya usajili wa shirika iambatishwe kwenye maombi ya TIN pamoja na Mkataba na Kanuni za Kampuni wakati mtu anapopeleka maombi TRA.

     

    Kampuni yenye dhima ya ukomo itaomba kupatiwa hati ya TIN kwa kujaza fomu za maombi kama ifuatavyo:

    • Maombi kwa ajili ya kampuni.
    • Maombi kwa ajili ya wanahisa/wakurugenzi, iwapo mkurugenzi yeyote kati yao ameshapatiwa hati ya TIN kwa madhumuni mengine anaweza kutoa maombi mengine. Namba ileile ya TIN itatumika.
    • Kwa wakurugenzi ambao si raia wanapaswa kutimiza masharti yote ya uhamiaji na kupata kibali cha biashara kutoka Idara ya Uhamiaji inayofanya kazi chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani.

     

         Ubia

    Wabia wanatakiwa kusajili kampuni katika ofisi za BRELA na kupata hati ya usajili ambayo inaonyesha namba na majina ya wabia pamoja na mgawanyo wa hisa zao.

    • Katika kutoa maombi ya TIN kampuni ya ubia itaomba kupatiwa hati kwa kuwasilisha nakala ya usajili waliyopata BRELA.
    • Kila mbia ataomba kupatiwa TIN, iwapo mbia yeyote tayari ameshapatiwa hati ya TIN kwa madhumuni mengine hatakiwi kutoa maombi mengine. Namba ileile ya TIN itatumika.

     

     Udhamini

    Udhamini ni mpango ambapo wadhamini wanamiliki mali lakini haihusishi ubia na kampuni.

    Amana inapaswa kusajiliwa kama kampuni katika ofisi za BRELA na kupata hati ya usajili ambayo inaonesha majina na anwani za wadhamini. Kila mdhamini anapaswa kuomba kupatiwa hati ya TIN, iwapo mdhamini yeyote kati yao akiwa ameshapatiwa hati ya TIN kwa madhumuni mengine hawezi kutuma maombi mengine. Namba ya TIN aliyo nayo itatumika.

     

    Shirika la msaada:

    Shirika hili litatambulika kama shirika la msaada kwa madhumuni ya masuala ya kodi baada ya kupatiwa kibali na Kamishna Mkuu. Mwombaji anatakiwa kupata nyaraka zote muhimu kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani.

     

    Tamko la Makadirio ya Mapato

    Utatakiwa kutoa tamko la makadirio ya mapato kwa ajili ya kufanyiwa makadirio  ya awali ya kodi kwa mwaka husika. Afisa wa kodi anaweza kukuhoji na kurekodi taarifa za biashara yako na taarifa zako binafsi katika ofisi ya TRA.

    See less
    • 0
    • Share
      Share
      • Share on WhatsApp
      • Share on Facebook
      • Share on Twitter
      • Report
  6. Promo – MeridianBet

    Kubet kumerahisishwa

    Jipatie Tsh 3,500 ya kuanzia kama zawadi ya kujiunga.

    Jiunge Sasa
  7. Asked: January 10, 2020Biashara/Ujasiriamali, TRA

    Nawezaje kupata TIN kwa ajili ya biashara yangu?

    Salim Jumbe

    Salim Jumbe

    • Dar es Salaam, Tanzania
    • 0 Questions
    • 127 Answers
    • 0 Best Answers
    • 436 Points
    View Profile
    Salim Jumbe Proffesional
    Jibu - January 10, 2020 saa 6:15 am
    Jibu hili limerekebishwa.

    Masharti: Picha ya pasipoti Kadi ya kitambulisho/ kitambulisho cha kazi   Taratibu: Wasilisha ombi la namba ya utambulisho wa ulipa kodi Kamilisha Fomu ya Maombi ya TIN (Nakala halisi) Chukua taarifa ya makadirio (chombo kinachoomba TIN) (Nakala halisi) Jaza fomu ya udhibitisho wa mlipa kodi (nSoma Zaidi

    Masharti:

    • Picha ya pasipoti
    • Kadi ya kitambulisho/ kitambulisho cha kazi

     

    Taratibu:

    • Wasilisha ombi la namba ya utambulisho wa ulipa kodi
    • Kamilisha Fomu ya Maombi ya TIN (Nakala halisi)
    • Chukua taarifa ya makadirio (chombo kinachoomba TIN) (Nakala halisi)
    • Jaza fomu ya udhibitisho wa mlipa kodi (nakala halisi)
    • Wasilisha nyaraka za ombi la TIN katika kituo cha karibu cha kodi kwenye wilaya ambayo eneo la biashara yako ilipo
    • Toa alama za vidole  za utambulisho
    • Pata namba ya utambulisho wa mlipa kodi (TIN) na fomu ya tathmini ya kodi
    • Pata TIN yako
    See less
    • 0
    • Share
      Share
      • Share on WhatsApp
      • Share on Facebook
      • Share on Twitter
      • Report
  8. Promo – MeridianBet

    Kubet kumerahisishwa

    Jipatie Tsh 3,500 ya kuanzia kama zawadi ya kujiunga.

    Jiunge Sasa
  9. Asked: January 10, 2020Biashara/Ujasiriamali, Maana za Maneno, TRA

    TIN namba ni nini?

    Salim Jumbe

    Salim Jumbe

    • Dar es Salaam, Tanzania
    • 0 Questions
    • 127 Answers
    • 0 Best Answers
    • 436 Points
    View Profile
    Salim Jumbe Proffesional
    Jibu - January 10, 2020 saa 6:13 am

    Namba ya utambulisho wa mlipa kodi (TIN) ni namba ya  tarakimu tisa inayotumika kufuatilia namba na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa madhumuni ya kodi.

    Namba ya utambulisho wa mlipa kodi (TIN) ni namba ya  tarakimu tisa inayotumika kufuatilia namba na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa madhumuni ya kodi.

    See less
    • 0
    • Share
      Share
      • Share on WhatsApp
      • Share on Facebook
      • Share on Twitter
      • Report
  10. Promo – MeridianBet

    Kubet kumerahisishwa

    Jipatie Tsh 3,500 ya kuanzia kama zawadi ya kujiunga.

    Jiunge Sasa
  11. Asked: January 9, 2020Kodi, TRA

    Viwango vya kodi ya VAT vikoje?

    Salim Jumbe

    Salim Jumbe

    • Dar es Salaam, Tanzania
    • 0 Questions
    • 127 Answers
    • 0 Best Answers
    • 436 Points
    View Profile
    Salim Jumbe Proffesional
    Jibu - January 9, 2020 saa 6:34 am

    Kodi ya Ongezeko la Thamani(VAT)  hutozwa katika bidhaa na huduma stahiki kwa viwango vifuatavyo :-   Na.   Viwango vya VAT Aina ya bidhaa na au huduma zinazohusika   Kiwango cha VAT 1 Bidhaa na huduma zinazotozwa kodi - Tanzania bara 18% 2 Uagizaji na uingizaji wa bidhaa na huduma toka nje kuingiaSoma Zaidi

    Kodi ya Ongezeko la Thamani(VAT)  hutozwa katika bidhaa na huduma stahiki kwa viwango vifuatavyo :-

     

    Na.

     

    Viwango vya VAT Aina ya bidhaa na au huduma zinazohusika

     

    Kiwango cha VAT

    1 Bidhaa na huduma zinazotozwa kodi – Tanzania bara 18%
    2 Uagizaji na uingizaji wa bidhaa na huduma toka nje kuingia Tanzania bara. 18%
    3 Uuzaji wa bidhaa nje ya nchi. 0%
    4 Kutomhusisha mpitishaji bidhaa kulipa VAT kwa gharama ya huduma ya usafirishaji wa bidhaa/mizigo iendayo nje ya nchi kupitia Tanzania Bara, huduma zinajumuisha:-
           I.        Huduma zinazohusiana moja kwa moja na bidhaa inayopitishwa kwenda nje ya nchi

     

    0%
           I.        Bidhaa zilizohifadhiwa kwenye bandari, uwanja wa ndege au maeneo ya forodha kwa kipindi kisichozidi siku 30 zikisubiri kusafirishwa  

    0%

    See less
    • 0
    • Share
      Share
      • Share on WhatsApp
      • Share on Facebook
      • Share on Twitter
      • Report
  12. Promo – MeridianBet

    Kubet kumerahisishwa

    Jipatie Tsh 3,500 ya kuanzia kama zawadi ya kujiunga.

    Jiunge Sasa
  13. Asked: January 8, 2020Kodi, TRA

    Kodi ya ongezeko la thamani(VAT) inatozwaje?

    Salim Jumbe

    Salim Jumbe

    • Dar es Salaam, Tanzania
    • 0 Questions
    • 127 Answers
    • 0 Best Answers
    • 436 Points
    View Profile
    Salim Jumbe Proffesional
    Jibu - January 8, 2020 saa 10:05 am

    Kila mtu aliyesajiliwa kwenye Kodi ya Ongezeko la Thamani katika mlolongo kati ya msambazaji wa kwanza na mnunuzi au mtumiaji wa mwisho, anatozwa kodi kwenye bidhaa alizouziwa (kodi kwenye manunuzi) na atatoza kodi kwa bidhaa atakazo uza (kodi kwenye mauzo). Analipa Mamlaka ya Mapato ziada ya kodi kSoma Zaidi

    Kila mtu aliyesajiliwa kwenye Kodi ya Ongezeko la Thamani katika mlolongo kati ya msambazaji wa kwanza na mnunuzi au mtumiaji wa mwisho, anatozwa kodi kwenye bidhaa alizouziwa (kodi kwenye manunuzi) na atatoza kodi kwa bidhaa atakazo uza (kodi kwenye mauzo). Analipa Mamlaka ya Mapato ziada ya kodi kwenye mauzo juu ya kodi kwenye manunuzi, au anarudishiwa ziada ya kodi kwenye manunuzi juu ya kodi kwenye mauzo. Katika mfumo huu biashara huwa haziathiriki isipokuwa mfanyabiashara anatakiwa kukusanya kodi hiyo kutoka kwa mnunuzi na kuiwasilisha TRA.

    See less
    • 0
    • Share
      Share
      • Share on WhatsApp
      • Share on Facebook
      • Share on Twitter
      • Report
  14. Promo – MeridianBet

    Kubet kumerahisishwa

    Jipatie Tsh 3,500 ya kuanzia kama zawadi ya kujiunga.

    Jiunge Sasa
  15. Asked: November 21, 2019Kodi, TRA

    VAT ni nini?

    Salim Jumbe

    Salim Jumbe

    • Dar es Salaam, Tanzania
    • 0 Questions
    • 127 Answers
    • 0 Best Answers
    • 436 Points
    View Profile
    Salim Jumbe Proffesional
    Jibu - November 21, 2019 saa 9:54 am

    VAT ni kifupi cha Value Added Tax, kwa kiswahili ni Kodi ya Ongezeko la thamani. Kodi ya Ongezeko la Thamani ni nini? Kodi ya Ongezeko  la Thamani ni kodi ya mlaji inayotozwa katika bidhaa zinazostahili kutozwa kodi, ikiwa ni pamoja na huduma, mali zisizohamishika na shughuli yoyote ya kiuchumi wakaSoma Zaidi

    VAT ni kifupi cha Value Added Tax, kwa kiswahili ni Kodi ya Ongezeko la thamani.

    Kodi ya Ongezeko la Thamani ni nini?

    Kodi ya Ongezeko  la Thamani ni kodi ya mlaji inayotozwa katika bidhaa zinazostahili kutozwa kodi, ikiwa ni pamoja na huduma, mali zisizohamishika na shughuli yoyote ya kiuchumi wakati wowote thamani inapoongezeka katika kila hatua ya uzalishaji na katika hatua ya mwisho ya mauzo. Kodi ya Ongezeko  la Thamani  inatozwa kwa bidhaa zote zinazozalishwa ndani na huduma na kwenye maduhuli. Kodi ya Ongezeko la Thamani anatozwa mtu aliyesajiliwa kulipa Kodi ya Ongezeko  la Thamani  tu.

    Mawanda ya Kodi ya Ongezeko  la Thamani  ni yapi?

    Kodi ya Ongezeko  la Thamani  itatozwa katika usambazaji wowote wa bidhaa, huduma na bidhaa zisizohamishika za shughuli yoyote ya kiuchumi Tanzania Bara ambapo ni usambazaji unaotozwa kodi unaofanywa na mlipa kodi katika shughuli ya kiuchumi anayofanya. Uingizaji wa bidhaa zinazokatwa kodi kutoka sehemu yoyote nje ya Tanzania Bara zitatozwa Kodi ya Ongezeko  la Thamani  na Sheria za Kawaida za Forodha na taratibu zitatumika. Bidhaa zote zitakazotumika nje ya Tanzania Bara hazitatozwa Kodi ya Ongezeko  la Thamani  baada ya kupata uthibitisho. Kodi ya Ongezeko  la Thamani  itatozwa kwa bidhaa na huduma zinazotozwa kodi. Viwango sanifu vya Kodi ya Ongezeko  la Thamani ni 18% na 0% kwa bidhaa zinazosafirishwa nje ya nchi.

    See less
    • 0
    • Share
      Share
      • Share on WhatsApp
      • Share on Facebook
      • Share on Twitter
      • Report
Adv

Sidebar

Uliza Swali

Promo

  • Usihangaike tena, Tumekuwekea Kampuni zote za kubet katika app moja! Jaribu Sasa

  • Beti kwa mara ya kwanza, ukishindwa unarudishiwa hela yako

  • Tafuta Ajira kiurahisi. Jaribu Sasa

  • Jifunze jinsi ya kubet kibingwa

  • Explore

    • Home
    • Maswali
    • Polls
    • Points
    • Watumiaji
    • Miongozo
    • App

    MojaSky | Designed by ChuiTec.