Jiunge

Jiunge MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection

Unayo account ? Log In

Unayo account ? Log in

Log In

Login MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection

Jiunge Hapa

Umesahau Password?

Hauna Account, Jiunge Hapa

Umesahau Password

Umesahau password yako?. Andika email yako hapo chini alafu bonyeza 'Reset'. Utapokea link katika email yako kwa ajili ya kutengeneza password mpya.

Unayo account ? Log in

Tafadhali andika jina lako kamili.

Tafadhali andika E-Mail yako.

Please choose an appropriate title for the question so it can be answered easily.

Tafadhali elezea kwa nini unahisi chapisho hili linapaswa kuripotiwa

Sign InSign Up

1Sky

1Sky

1Sky Navigation

  • Blog
  • Wasiliana Nasi
  • Advanced Search
  • App

Mobile menu

Close
Uliza Swali
  • Home
  • Maswali
  • Points
  • Miongozo
  • Wasiliana Nasi
  • Advanced Search
  • App
Home» Maswali»Q 34693
In Process
Adv
Anonymous
Asked: January 16, 20202020-01-16T13:38:49+03:00 2020-01-16T13:38:49+03:00Wazazi

Nifanyeje ili mtoto wangu asiwe anadanganya?

Nifanyeje ili mtoto wangu asiwe anadanganya?
  • 1
  • 270
  • 0
  • Share
    • Share on WhatsApp
    • Share on Facebook
    • Share on Twitter
Jibu
  • Report
Adv

Jibu 1

  • Kura
  • Zamani
  • Mpya
  1. Salim Jumbe

    Salim Jumbe

    • Dar es Salaam, Tanzania
    • 0 Questions
    • 127 Answers
    • 0 Best Answers
    • 430 Points
    View Profile
    Salim Jumbe Proffesional
    2020-01-16T13:43:23+03:00Jibu - January 16, 2020 saa 1:43 pm

    Zingatia haya
     
    Sababu za watoto kudanganya
    Umri. Mtoto mwenye miaka pungufu ya mitatu, kwa mfano, hana uwezo wa kusema uongo. Hata pale anapoonekana kudanganya, kimsingi hakusudii kudanganya kwa sababu akili yake haina uwezo wa kutunga uongo. Kinachoonekana kuwa uongo ni kusema kile anachotamani kingekuwa.
     
    Vile vile, mtoto hudanganya kwa lengo la kukwepa matokeo ya kusema ukweli utakaomgharimu. Kwa sababu mara nyingi matokeo hayo ni pamoja na adhabu, mtoto hutumia uongo kama namna ya kujihami awe salama.
     
    Je, tunawezaje kumsaidia mtoto kuwa mkweli? Ingawa zipo namna nyingi, hapa nina mapendekezo makubwa matatu yanayohusiana.
     
    Usimdanganye
    Tabia ya mtoto ni sura ya kile anachokifanya mzazi wake. Ikiwa unataka mtoto wako asikudanganye, basi anza kwa kuwa mkweli kwake. Unapoahidi kumletea zawadi, kwa mfano, usiache kutekeleza ahadi yako.
     
    Aidha, usitumie uongo kumridhisha mtoto. Anapouliza swali gumu, mpe maelezo rahisi ya kweli badala ya uongo ‘mzuri’ ambao, hata hivyo, anaweza kuugundua baadae. Anapogundua ulimdanganya, ni rahisi kuuona uongo kuwa tabia ya kawaida.
     
    Usimwadhibu kwa kusema ukweli
    Unafanyaje mtoto anapokwambia ukweli usioupenda? Je, unamwadhibu kwa sababu amekosea? Ukweli ni kwamba kumwadhibu mtoto kwa kukuambia ukweli ni sawa na kumwambia, ‘katika maisha ni hatari kuwa mkweli’. Hivyo, ni vizuri kuweka mazingira ya mtoto kujua kuwa ni afadhali kusema ukweli pale tunapokosea kuliko kufunika makosa kwa kutumia uongo.
     
    Pia, kutokumwadhibu kwa kukiri kosa, kwa mfano, ni motisha ya kujisikia anaweza kusema ukweli na bado uhusiano wake na wewe mzazi usiathirike.
     
    Usiweke mazingira ya kudanganywa
    Kama tayari unajua mtoto amefanya kosa, haina sababu ya kumwuuliza maswali ya mtego yanayotafuta majibu ambayo tayari unayajua. Kwa mfano, kama ulitarajia mtoto alale mchana na umegundua hajalala, usiombe kudanganywa kwa kuuliza swali kama, “hivi umelala leo?” Badala ya kumfanya alazimike kudanganya, ni vyema kushughulikia kosa moja kwa moja kwa lugha inayojenga badala ya kuuliza maswali yasiyosaidia kutatua tatizo na yanayokaribisha uongo.
     
    Kadhalika, usimwite mtoto ‘mwongo’ hata kama amekudanganya. Majina ya ‘wewe ni mwongo’, ‘nilijua tu utanidanganya’ hujenga taswira ya kujiona uongo ni sehemu ya maisha yake. Tumia lugha yenye kuonesha matarajio chanya hata pale unapogundua umedanganywa.
     
    Kukosea ni sehemu ya maisha
    Kwa ujumla, ni vyema kumfundisha mtoto kwamba kukosea si jambo baya katika maisha. Makosa ni fursa ya kujirekebisha yanaposhughulikiwa vizuri. Hakuna sababu ya kumfanya mtoto ajifunze kufukia makosa yake kwa uongo.
     

    Nukuu kutoka BwayaBlog

    • 0
    • Reply
    • Share
      Share
      • Share on WhatsApp
      • Share on Facebook
      • Share on Twitter
      • Report
Jibu swali hili

Jibu swali hili
Cancel reply

Chagua
Captcha Click on image to update the captcha.

Adv

Sidebar

Uliza Swali

Promo

  • Usihangaike tena, Tumekuwekea Kampuni zote za kubet katika app moja! Jaribu Sasa

  • Beti kwa mara ya kwanza, ukishindwa unarudishiwa hela yako

  • Tafuta Ajira kiurahisi. Jaribu Sasa

  • Jifunze jinsi ya kubet kibingwa

  • Maswali yanayoendana

    • Nifanyeje ili mtoto wangu anisikilize na kuniamini?

    Explore

    • Home
    • Maswali
    • Polls
    • Points
    • Watumiaji
    • Miongozo
    • App

    MojaSky | Designed by ChuiTec.

    Insert/edit link

    Enter the destination URL

    Or link to existing content

      No search term specified. Showing recent items. Search or use up and down arrow keys to select an item.