Nifanyeje ili mtoto wangu asiwe anadanganya?
Jiunge MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection
Login MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection
Umesahau password yako?. Andika email yako hapo chini alafu bonyeza 'Reset'. Utapokea link katika email yako kwa ajili ya kutengeneza password mpya.
Tafadhali elezea kwa nini unahisi chapisho hili linapaswa kuripotiwa
Salim Jumbe
Zingatia haya
Sababu za watoto kudanganya
Umri. Mtoto mwenye miaka pungufu ya mitatu, kwa mfano, hana uwezo wa kusema uongo. Hata pale anapoonekana kudanganya, kimsingi hakusudii kudanganya kwa sababu akili yake haina uwezo wa kutunga uongo. Kinachoonekana kuwa uongo ni kusema kile anachotamani kingekuwa.
Vile vile, mtoto hudanganya kwa lengo la kukwepa matokeo ya kusema ukweli utakaomgharimu. Kwa sababu mara nyingi matokeo hayo ni pamoja na adhabu, mtoto hutumia uongo kama namna ya kujihami awe salama.
Je, tunawezaje kumsaidia mtoto kuwa mkweli? Ingawa zipo namna nyingi, hapa nina mapendekezo makubwa matatu yanayohusiana.
Usimdanganye
Tabia ya mtoto ni sura ya kile anachokifanya mzazi wake. Ikiwa unataka mtoto wako asikudanganye, basi anza kwa kuwa mkweli kwake. Unapoahidi kumletea zawadi, kwa mfano, usiache kutekeleza ahadi yako.
Aidha, usitumie uongo kumridhisha mtoto. Anapouliza swali gumu, mpe maelezo rahisi ya kweli badala ya uongo ‘mzuri’ ambao, hata hivyo, anaweza kuugundua baadae. Anapogundua ulimdanganya, ni rahisi kuuona uongo kuwa tabia ya kawaida.
Usimwadhibu kwa kusema ukweli
Unafanyaje mtoto anapokwambia ukweli usioupenda? Je, unamwadhibu kwa sababu amekosea? Ukweli ni kwamba kumwadhibu mtoto kwa kukuambia ukweli ni sawa na kumwambia, ‘katika maisha ni hatari kuwa mkweli’. Hivyo, ni vizuri kuweka mazingira ya mtoto kujua kuwa ni afadhali kusema ukweli pale tunapokosea kuliko kufunika makosa kwa kutumia uongo.
Pia, kutokumwadhibu kwa kukiri kosa, kwa mfano, ni motisha ya kujisikia anaweza kusema ukweli na bado uhusiano wake na wewe mzazi usiathirike.
Usiweke mazingira ya kudanganywa
Kama tayari unajua mtoto amefanya kosa, haina sababu ya kumwuuliza maswali ya mtego yanayotafuta majibu ambayo tayari unayajua. Kwa mfano, kama ulitarajia mtoto alale mchana na umegundua hajalala, usiombe kudanganywa kwa kuuliza swali kama, “hivi umelala leo?” Badala ya kumfanya alazimike kudanganya, ni vyema kushughulikia kosa moja kwa moja kwa lugha inayojenga badala ya kuuliza maswali yasiyosaidia kutatua tatizo na yanayokaribisha uongo.
Kadhalika, usimwite mtoto ‘mwongo’ hata kama amekudanganya. Majina ya ‘wewe ni mwongo’, ‘nilijua tu utanidanganya’ hujenga taswira ya kujiona uongo ni sehemu ya maisha yake. Tumia lugha yenye kuonesha matarajio chanya hata pale unapogundua umedanganywa.
Kukosea ni sehemu ya maisha
Kwa ujumla, ni vyema kumfundisha mtoto kwamba kukosea si jambo baya katika maisha. Makosa ni fursa ya kujirekebisha yanaposhughulikiwa vizuri. Hakuna sababu ya kumfanya mtoto ajifunze kufukia makosa yake kwa uongo.
Nukuu kutoka BwayaBlog