Ndoa ni nini?
Jiunge MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection
Login MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection
Umesahau password yako?. Andika email yako hapo chini alafu bonyeza 'Reset'. Utapokea link katika email yako kwa ajili ya kutengeneza password mpya.
Tafadhali elezea kwa nini unahisi chapisho hili linapaswa kuripotiwa
Ndoa ni muungano wa kijamii au mkataba wa kisheria kati ya watu wanaojulikana kuwa wanandoa. Katika tamaduni mbalimbali, ndoa zinakamilishwa kwa sherehe ya ndoa.
Promo – AjiraSearch
Ajira ya Ndoto Yako
Sasa kutafuta ajira ni rahisi zaidi kwa kutumia app hii.
Tazama AppEmmanuel Magessa
Ndoa ni agano lenye kusudi la wawili (Mwanamume na mwanamke) kuishi pamoja kama mwili mmoja maisha yao yote baada ya kukubaliana, kila mmoja akimkubali mwenzake kuishi na kuwa naye wakati wote ktk hali zote kwa moyo wake wote.
Katika ngazi hii ya mahusiano ndipo watu huwa mke na mume kwa kuunganishwa na Mungu kuwa mwili mmoja. Na ktk ngazi hii tendo la ndoa uhusika, na mambo yote ya faragha yahusuyo upendo, na si ktk uchumba. Huwezi kuishi maisha ya ndoa wakati wa uchumba; ukashiriki tendo la ndoa, na kufanya mambo ya faragha ya upendo na yale yasiyo ya faragha lkn yanawahusu zaidi wana ndoa. Kufanya hivyo ni kuharibu ndoa yenu, lkn kuhatarisha mahusiono yako ya uchumba.
Unaposhiriki mambo ya ndoa wakati wa uchumba unajijengea na unamjengea mwenzi wako tabia ya kukosa uaminifu ktk ndoa yenu na hivyo kuwa wachepukaji wakati wa ndoa. Lakini pia kufanya hivyo ni kumpa ibilisi nafasi ktk uchumba wenu, na lazima ataharibu tu, asipoharibu kwenye uchumba ataharibu kwenye ndoa, hawezi kuwaacha ivi hivi ikiwa mmempa nafasi. Na kati ya watu wanatumia nafasi bila kupoteza iwapo wataipata, ni shetani. Kwa hiyo kuwa mwangalifu sana.
Usipoteze uzaliwa wako wa kwanza na mbaraka wako kwa kipande cha mkate ambacho utamu wake haudumu kinywani na ujazo wake haujazi tumbo milele. Japokuwa ni kitamu kitatupwa chooni na wala hutabaki chooni ukifurahi kukitazama. Jitunze, mtunze mwenzi wako, tunza uchumba wako, tunza ndoa yako. Matunzo yanaanza kwa wewe kujitunza, kumtunza mwenzi wako, kutunza uchumba wako na hatimaye kutunza ndoa yako.
kutoka hebroni blog