Jiunge

Jiunge MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection

Unayo account ? Log In


Unayo account ? Log in

Log In

Login MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection

Jiunge Hapa


Umesahau Password?

Hauna Account, Jiunge Hapa

Umesahau Password

Umesahau password yako?. Andika email yako hapo chini alafu bonyeza 'Reset'. Utapokea link katika email yako kwa ajili ya kutengeneza password mpya.

Unayo account ? Log in

Tafadhali andika jina lako kamili.

Tafadhali andika E-Mail yako.

Please choose an appropriate title for the question so it can be answered easily.


Tafadhali elezea kwa nini unahisi chapisho hili linapaswa kuripotiwa

Sign InSign Up

1Sky

1Sky

1Sky Navigation

  • Blog
  • Wasiliana Nasi
  • Advanced Search
  • App

Mobile menu

Close
Uliza Swali
  • Home
  • Maswali
  • Points
  • Miongozo
  • Wasiliana Nasi
  • Advanced Search
  • App
Home» Maswali»Q 34763
In Process
Anonymous
Asked: January 22, 20202020-01-22T14:39:11+03:00 2020-01-22T14:39:11+03:00Elimu

Nawezaje kukumbuka nilichokisoma?

Nawezaje kukumbuka nilichokisoma?
  • 1
  • 400
  • 0
  • Share
    • Share on WhatsApp
    • Share on Facebook
    • Share on Twitter
Jibu
  • Report

Jibu 1

  • Kura
  • Zamani
  • Mpya
  1. Calvin Mlay

    Calvin Mlay

    • Dar es Salaam, Tanzania
    • 0 Questions
    • 81 Answers
    • 0 Best Answers
    • 385 Points
    View Profile
    Calvin Mlay Proffesional
    2020-01-22T14:45:44+03:00Jibu - January 22, 2020 saa 2:45 pm

    Kukumbuka ni uwezo wa kuzipata taarifa ulizozihifadhi akilini ili uweze kuzitumia pale unapozihitaji. Kwa mfano unapokutana na mtu uliyekutana naye miaka kumi iliyopita na kuweza kupata jina lake katika fahamu zako na ukamwita kwa jina lake, hapo umekumbuka. 

    Kwa kawaida, akili ya mwanadamu haikumbuki kila taarifa. Huchagua kipi cha kusahaulika na kipi cha kukumbuka. Ndio maana tunaona mengi lakini tunakumbuka yale machache ambayo akili inayapa uzito.

    Makala haya, kwa kutumia uchambuzi wa tafiti mbalimbali za elimu ya kujifunza, yanapendekeza mbinu sita kukuwezesha kukumbuka.

     

    Furahia unachotaka kukikumbuka

    Jitahidi kufurahia kile unachojifunza. Penda masomo yako. Kama unasoma Hisabati, anza kwa kuipenda. Unapopenda kile unachokisoma, unaongeza uwezekano wa kukikumbuka. Usipopenda masomo, itakuwa rahisi kusahau.

    Fahamu wazo kuu kabla ya undani

    Anza kwa kuelewa wazo kuu la kile unachojifunza kabla hujaweka nguvu kuelewa undani wake. Unapoelewa maarifa ya jumla kwanza, unajenga msingi wa hatua ya pili ya kuingiza taarifa za kina kujazia kile ambacho tayari akili yako inakijua.

    Tafuta mfanano na utofauti wa dhana

    Unapoingiza taarifa isiyofanana na kile unachofahamu, utatumia nguvu nyingi bila sababu. Kwa hivyo unashauriwa kusoma kidogo kidogo kwa kuhusianisha kile unachokisoma na kile unachokifahamu ili kurahisisha kazi ya akili kupangilia mambo kukuwezesha kuelewa.

    Oanisha unachokisoma na maisha halisi

    Unapopita barabarani, kwa mfano, unakutana na watu wengi ambao kimsingi huwezi kuwakumbuka. Lakini unapokutana na mtu anayehusiana na maisha yako, ni rahisi kumkumbuka.

    Jaribu kuhusianisha maarifa unayojifunza na maisha yako ya kila siku. Kama huwezi kuona namna gani hayo unayoyasoma yanahusiana na maisha yako ya kila siku, lazima utasahau.

    Tumia maarifa unayojifunza

    Jenga tabia ya kutumia maarifa yako. Andika kila unaposoma. Fundisha wenzako. Jadili na wenzako. Fanya maswali mara kwa mara. Kufanya hivyo, kunakusaidia kuyamiliki maarifa uliyonayo na hivyo kurahisisha kazi ya kukumbuka.

    Inapobidi, kariri

    Jifunze mbinu za kukariri kwa urahisi. Rudia rudia kile unachotaka kukikumbuka. Unaporudia rudia jambo hata kama hulielewi, unaongeza nafasi ya kulikumbuka. Unaweza pia kutumia herufi za mwanzo za orodha ya hoja unazotaka kuzikumbuka kutengeneza maneno unayoweza kuyakumbuka kirahisi.

    Nimeitoa katika blog ya Bwaya, ukitaka kusoma kwa urefu zaidi ingia hapa

    • 0
    • Reply
    • Share
      Share
      • Share on WhatsApp
      • Share on Facebook
      • Share on Twitter
      • Report
Jibu swali hili

Jibu swali hili
Cancel reply

Chagua

Sidebar

Promo

  • Gugo kwa Kiswahili, Jaribu Sasa

  • Nafasi zote mpya za kazi zipo hapa

  • Tafuta vitu mtandaoni kwa lugha ya Kiswahili

  • Tafuta Ajira kiurahisi. Jaribu Sasa

  • Maswali Mengine

    • kirefu cha NACTE ni nini?

      • Majibu 0
    • Masharti na taratibu za kuomba mkopo Bodi ya Mikopo HESLB zikoje?

      • Jibu 1
    • Kama siwafahamu wazazi wangu najaza nini katika fomu ya bodi ya mikopo?

      • Jibu 1
    • Contacts za Ruaha Catholic University ni zipi?

      • Jibu 1
    • Vyuo vilivyosajiliwa na NACTE ni vipi?

      • Jibu 1
    • Inachukua muda gani fomu ya bodi ya mkopo kufunguka baada ya kulipa?

      • Jibu 1
    • Contact za Chuo cha Mipango ni zipi?

      • Jibu 1
    • Unazo contacts za Arusha Technical College?

      • Jibu 1
    • Faculty za Chuo Kikuu cha Ruaha ni zipi?

      • Jibu 1
    • Contacts za CBE ni zipi?

      • Jibu 1

    Explore

    • Home
    • Maswali
    • Polls
    • Points
    • Watumiaji
    • Miongozo
    • App

    MojaSky

    Insert/edit link

    Enter the destination URL

    Or link to existing content

      No search term specified. Showing recent items. Search or use up and down arrow keys to select an item.