Nawezaje kukumbuka nilichokisoma?
Jiunge MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection
Login MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection
Umesahau password yako?. Andika email yako hapo chini alafu bonyeza 'Reset'. Utapokea link katika email yako kwa ajili ya kutengeneza password mpya.
Tafadhali elezea kwa nini unahisi chapisho hili linapaswa kuripotiwa
Calvin Mlay
Kukumbuka ni uwezo wa kuzipata taarifa ulizozihifadhi akilini ili uweze kuzitumia pale unapozihitaji. Kwa mfano unapokutana na mtu uliyekutana naye miaka kumi iliyopita na kuweza kupata jina lake katika fahamu zako na ukamwita kwa jina lake, hapo umekumbuka.
Kwa kawaida, akili ya mwanadamu haikumbuki kila taarifa. Huchagua kipi cha kusahaulika na kipi cha kukumbuka. Ndio maana tunaona mengi lakini tunakumbuka yale machache ambayo akili inayapa uzito.
Makala haya, kwa kutumia uchambuzi wa tafiti mbalimbali za elimu ya kujifunza, yanapendekeza mbinu sita kukuwezesha kukumbuka.
Furahia unachotaka kukikumbuka
Jitahidi kufurahia kile unachojifunza. Penda masomo yako. Kama unasoma Hisabati, anza kwa kuipenda. Unapopenda kile unachokisoma, unaongeza uwezekano wa kukikumbuka. Usipopenda masomo, itakuwa rahisi kusahau.
Fahamu wazo kuu kabla ya undani
Anza kwa kuelewa wazo kuu la kile unachojifunza kabla hujaweka nguvu kuelewa undani wake. Unapoelewa maarifa ya jumla kwanza, unajenga msingi wa hatua ya pili ya kuingiza taarifa za kina kujazia kile ambacho tayari akili yako inakijua.
Tafuta mfanano na utofauti wa dhana
Unapoingiza taarifa isiyofanana na kile unachofahamu, utatumia nguvu nyingi bila sababu. Kwa hivyo unashauriwa kusoma kidogo kidogo kwa kuhusianisha kile unachokisoma na kile unachokifahamu ili kurahisisha kazi ya akili kupangilia mambo kukuwezesha kuelewa.
Oanisha unachokisoma na maisha halisi
Unapopita barabarani, kwa mfano, unakutana na watu wengi ambao kimsingi huwezi kuwakumbuka. Lakini unapokutana na mtu anayehusiana na maisha yako, ni rahisi kumkumbuka.
Jaribu kuhusianisha maarifa unayojifunza na maisha yako ya kila siku. Kama huwezi kuona namna gani hayo unayoyasoma yanahusiana na maisha yako ya kila siku, lazima utasahau.
Tumia maarifa unayojifunza
Jenga tabia ya kutumia maarifa yako. Andika kila unaposoma. Fundisha wenzako. Jadili na wenzako. Fanya maswali mara kwa mara. Kufanya hivyo, kunakusaidia kuyamiliki maarifa uliyonayo na hivyo kurahisisha kazi ya kukumbuka.
Inapobidi, kariri
Jifunze mbinu za kukariri kwa urahisi. Rudia rudia kile unachotaka kukikumbuka. Unaporudia rudia jambo hata kama hulielewi, unaongeza nafasi ya kulikumbuka. Unaweza pia kutumia herufi za mwanzo za orodha ya hoja unazotaka kuzikumbuka kutengeneza maneno unayoweza kuyakumbuka kirahisi.
Nimeitoa katika blog ya Bwaya, ukitaka kusoma kwa urefu zaidi ingia hapa