Masharti ya kujiunga kufanya mitihani ya ATEC I ni yapi?
Jiunge MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection
Login MojaSky ili uweze kuuliza maswali, kujibu maswali ya watu wengine na kutengeneza connection
Umesahau password yako?. Andika email yako hapo chini alafu bonyeza 'Reset'. Utapokea link katika email yako kwa ajili ya kutengeneza password mpya.
Tafadhali elezea kwa nini unahisi chapisho hili linapaswa kuripotiwa
Salim Jumbe
Masharti ya kujiunga katika mitihani ya ATEC ni kuwa na cheti cha kumaliza elimu ya Sekondari na kufaulu vizuri (credit) masomo yasiyopungua matatu (3) na kufaulu (pass grade) masomo mawili (2) ikiwemo Kiingereza na Hisabati.
AU cheti cha kumaliza elimu ya sekondari kidato cha sita (VI) na kufaulu masomo makuu mawili au moja na somo la ziada, alimradi uwe umefaulu Hisabati katika Elimu ya Sekondari ya Kidato cha nne (IV) angalau kwa alama ya D.
AU Cheti cha mwaka mmoja kutoka chuo kinachotambulika pamoja na ufaulu wa alama ya D au zaidi katika masomo ya Kiingereza na Hisabati katika cheti cha kidato cha nne
AU Vyeti vingine ambavyo vitakavyoendelea kutambuliwa na Bodi wakati kwa wakati.